Jaribio la mapinduzi visiwani Comoro
23 Aprili 2013Matangazo
Miongoni mwa waliokamatwa ni mtoto wa kiume wa rais wa zamani Ahmed Abdalla, ambaye aliuawa 1989. Juhudi za kuwapa maafisa wa serikali ya Comoro kuzungumzia kuhusu njama hiyo hazikufanikiwa, hata hivyo kiongozi wa upinzani nchini humo Houmed Msaidie ameilaumu serikali kwa kushindwa hadi sasa kutoa maelezo juu ya tukio hilo, ikiwa siku tatu baada ya watu hao kukamatwa. Daniel Gakuba amezungumza na bwana huyo, kusikiliza mahojiano hayo bonyeza alama ya kusikiliza masikioni hapo chini.
Mhariri: Mohammed Abdul-Rahman