Ireland kubana matumizi
25 Novemba 2010Matangazo
Serikali ya Ireland imetangaza hatua ngumu za kubana matumizi zenye lengo la kusaidia kutatua mzozo wa madeni wa nchi hiyo.
Pamoja na kupunguza matumizi na kuongeza kodi, kutakuwa na upunguzaji wa mshahara wa kima cha chini na ajira kwa maelfu ya wafanyakazi wa umma zitafutwa.
Mpango huo wa miaka minne unalenga kupunguza matumizi kwa kiasi Euro bilioni 15. Serikali hiyo pia inajadiliana kuhusu kupatiwa mkopo wa fedha na Umoja wa Ulaya na Shirika la Fedha la Kimataifa-IMF, unaotarajiwa kuwa na thamani ya karibu Euro bilioni 85.
Waziri Mkuu wa Ireland, Brian Cowen, ambaye serikali yake inakaribia kuvunjika, amedai kuwa mipango yake hiyo itarejesha tena imani iliyotoweka.