1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
MigogoroIran

Iran yaionya Marekani dhidi ya uvamizi wa aina yoyote

29 Januari 2026

Iran imesema itajibu vikali shambulizi lolote litakalofanywa na Marekani. Ujumbe wa Iran kwenye umoja huo umetoa onyo hilo jana Jumatano likijibu kitisho cha Rais Donald Trump cha kuiingilia kijeshi.

https://p.dw.com/p/57eOA
Iran Buschehr 2010 | Ufunguzi wa kinu cha kwanza cha nyuklia cha Iran
Kinu cha nyuklia cha Busheir kilichopo kusini mwa Iran wakati kikifunguliwa Agosti 21, 2010Picha: Abedin Taherkenareh/dpa/picture alliance

Ujumbe huo uliandika kwenye mtandao wa X kwamba Iran iko tayari kwa mazungumzo ya kuheshimiana na yenye maslahi kwa pande zote, lakini ikaonya ikiwa italazimishwa, itajilinda na kujibu vikali kuliko ilivyowahi kutokea.

Trump jana Jumatano alirudia tena kutoa vitisho vya kuishambulia Iran akisema muda unakwenda wa kufikia makubaliano ya nyuklia na kusema, kwa kuwa tayari aliitaka Iran kufikia makubaliano, lakini hawakufanya hivyo shambulizi litakalofuata litakuwa la maangamizi kwa taifa hilo.