Ibada ya kumuaga Isaac Gamba yaendelea Dar es Salaam
29 Oktoba 2018Ibada ya kumuaga mwandishi wa habari wa idhaa ya Kiswahili DW, Isaac Muyenjwa Gamba, inaendelea Lugalo mjini Dar es Salaam.
Mamia ya waombolezaji wamekusanyika katika eneo la hospitali ya jeshi ya Lugalo jijini Dar es Salaam kwa ajili ya kuuaga mwili wa mtangazaji Isaac Gamba aliyefariki dunia Ujerumani.
Watu mbalimbali, familia, jamaa, ndugu, marafiki , Mkuu wa Idhaa ya kiswahili ya DW pamoja na baadhi ya watumishi wa idhaa, waandishi wa habari wa vyombo vya kimataifa na kitaifa, wasikilizaji na waliokuwa wapendwa wa marehemu wamekusanyika eneo la hsopitali ya Lugalo kutoa heshima zao za mwisho.
Mwili wa Isaac Gamba uliwasili Dar es Salaam kutoka Ujerumani alfajiri ya leo.
Baadaye mwili wa marehemu utasafirishwa kuelekea Mwanza kisha hadi kijijini kwao Bunda kwa ajili ya mazishi ambayo Kwa mujibu wa msemaji wa familia huenda yakafanyika Jumatano.
Mhariri: Mohammed Abdul-Rahman