Aliyamaliza maisha yake mwenyewe akiwa na miaka 43 tu, lakini ni baada ya kuongoza mapambano ya kishujaa dhidi ya utawala wa Kijerumani. Jina lake halisi ni Mtwa Mkwava Mkwavinyika Ndevivalagosi Simkali Seligamba ama wengine wakimtaka Chifu Mkwavinyika Munyigumba Mwamuyinga. Alizaliwa mnamo mwaka 1855 na akafariki dunia tarehe 19 Julai 1898.