1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

HARARE:Twiga anusurika

22 Septemba 2007
https://p.dw.com/p/CBNY

Polisi nchini Zimbabwe waliwazuia wanakijiji kumchinja na kumla twiga mmoja aliyepoteza njia mjini Harare.Twiga huyo aliyekuwa pekee anaaminika kuingia mkoa wa kusini wa Seke kutoka shamba moja lililokuwa karibu.Uongozi wa mbuga za wanyama ulimuondoa twiga huyo baada ya polisi kuzuia umati wa watu kumuua na kumpika.Zimbabwe inakabiliwa na uhaba mkubwa wa nyama na bidhaa za matumizi kufuatia mkwamo wa kiuchumi na mfumko wa bei uliofikia takriban asilimia alfu 7.