Usawa wa kijinsia ni mojawapo ya malengo endelevu ya Umoja wa Mataifa pamoja na mengineyo ikiwemo kupiga vita njaa, umaskini na uwepo wa elimu bora. Katika makala ya Wanawake na Maendeleo, Anuar Mkama anaangazia harakati za kuwakomboa na kuwainua wanawake nchini Tanzania hususan katika kipindi hiki cha serikali ya awamu ya tano.