1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Hamilton ashinda Russian Grand Prix

12 Oktoba 2015

Bingwa wa sasa wa dunia wa mbio za magari ya Formula One Lewis Hamilton anakaribia kuhifadhi taji lake na kushinda ubingwa wa tatu wa dunia baada ya ushindi wake katika mbio za Russia Grand Prix

https://p.dw.com/p/1GmtI
Sotschi Russland Formel 1 Siegerehrung mit Putin
Picha: Getty Images/L. Baron

Lakini timu yake ya Mercedes tayari imeweka jicho moja katika msimu wa 2016 baada ya kuthibitishwa kuwa mabingwa wa taji la ujenzi kwa mwaka wa pili mfululizo.

Muingereza Hamilton sasa anaongoza msimamo wa madereva akiwa na pointi 302 mbele ya Sebastian Vettel wa Ferrari ambaye ana pointi 236 naye Nico Rosberg wa Mercedes akiwa na 229.

Ushindi wa jana ulikuwa wa 42 kwa Hamilton katika Formula One na kumpiku gwiji wa mashindano hayo Aryton Senna.

Mwandishi: Bruce Amani/AFP/DPA/AP/Reuters
Mhariri: Iddi Ssessanga