Hali ya kisiasa nchini Kenya
15 Mei 2012Matangazo
Wagombea urais, Uhuru Kenyata, Musalia Mudavad, William Ruto na Peter Kenneth wamekuwa miongoni mwa wabunge walio katika hatari ya kupoteza wadha huo baada ya kuasi vyama vyao ambavyo viliwaingiza bungeni. Kundi lenye mfungamano na Waziri Mkuu wa taifa hilo, Raila Odinga, limekwenda mahakamani kutaka amri ya kuondolewa kwa viongozi hao.
Sudi Mnette amezungumza na makamu mwenyekiti wa kundi lilowasilisha shtaka hilo mahakamani, Hassan Omar Hassan, na kwanza alimuuliza kikatiba kipi kimekiukwa?
(Kusikiliza mazungumzo hayo bonyeza alama ya spika za masikioni hapo chini)
Mwandishi: Sudi Mnette
Mhariri: Miraji Othman