Global Media Forum 2014
14 Aprili 2014Matangazo
Tovuti (World Wide Web) imekuwa msingi wa mawasiliano ya dunia, katika nyanja za uchumi, sayansi na siasa. Imefungua mlango kwa mamilioni ya watu na kuwapa fursa ya kushiriki katika masuala ambayo yako mbali ya mipaka ya jamii zao. Enzi ya digitali imeleta fursa, lakini pia inaambatana na hatari. Matumizi mabaya ya internet yanatokea katika mitindo mbali mbali, kama vile uhalifu wa kimtandao, na kupambana na changamoto hizo kunahitaji juhudi za pamoja kati ya watunga sera na makampuni ya biashara. Deutsche Welle inatarajia kuwa watu zaidi ya 2000 watashiriki kwenye mjadala kuhusu suala hili.
Bonyeza hapa kupata maelezo mengine: www.dw.de/globalmediaforum