1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

GAZA.Wanajeshi wa Israel wamewauwa watu wanne

12 Oktoba 2006
https://p.dw.com/p/CD3b

Majeshi ya Israel yamewauwa wapalestina watano akiwemo mtoto wakati yaliposhambulia Ukanda wa Gaza.

Majeshi hayo ya Israel yakipewa ulinzi na ndege za helikopta yaliingia katika kijiji cha Abassan katika operesheni ya kumsaka mwanajeshi wao aliyetekwa nyara miezi minne iliyopita.

Kwa mujibu wa jeshi la Israel Wanajeshi wake walilazimika kujibu mashambulio wakati waliposhambuliwa na wapiganaji wa Kipalestina.