1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

GAZA: Shule ya Umoja wa Mataifa yashambuliwa

7 Mei 2007
https://p.dw.com/p/CC4D

Mtu mmoja ameuawa na wengine 6 wamejeruhiwa baada ya mtu mwenye bunduki kufyatua risasi katika shule inayoongozwa na Umoja wa Mataifa katika Ukanda wa Gaza.Afisa mmoja amesema,washukiwa 3 wamekamatwa.Kwa mujibu wa maafisa,shambulio hilo lililofanywa na wafuasi wa kundi lenye itikadi kali za kidini,lililenga sherehe ya michezo ya spoti ya shule hiyo,iliyohudhuriwa na wasichana na wavulana.