1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Feri mbili zaanza kufanya kazi katika kivuko cha Likoni, Mombasa

Josephat Nyiro Charo14 Juni 2010

Kivuko cha Likoni kimekabiliwa na msongamano mkubwa wa magari hivyo kuathiri biashara ya utalii katika hoteli zilizoko kusini mwa jiji la Mombasa

https://p.dw.com/p/NqZj

Huduma za uchukuzi katika kivuko cha Likoni mjini Mombasa, Kenya sasa zinatarajiwa kuimarika baada ya feri mbili kubwa zilizoundwa nchini Ujerumani kukabidhiwa rasmi kwa serikali ya Kenya.

Feri hizo mbili zilizowasili nchini humo wiki mbili zilizopita, zinatarajiwa kupunguza kwa kiwango kikubwa msongamano, mbali na kuimarisha uchumi na biashara baina ya Kenya na Nchi Jirani ya Tanzania. Mwandishi wetu Eric Ponda kutoka Mombasa na taarifa zaidi.