1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

FC Kolon yachungulia daraja la pili

Sekione Kitojo
23 Aprili 2018

Hakuna jicho lililokosa  machozi  jana  mjini  Kolon wakati  FC Kolon ilipotumbukia  katika shimo la  kushuka  daraja  ...  wakati Hamburg SV yapata  matumaini  kwa  mbali  ya  kubakia  katika  Bundesliga.

https://p.dw.com/p/2wWaS
1. Bundesliga | 1. FC Koeln v FC Schalke 04 (2:2)
Picha: picture-alliance/dpa/F. Gambarini

Schalke 04  imeweka  mguu  mmoja  katika  michuano  ya Champions League  msimu  ujao wakati  FC Kolon  iko katika  ukingo wa  kushuka  daraja  baada  ya  sare  ya  mabo  2-2  jana  Jumapili. Wachezaji  pamoja  na  mashabiki  wa FC Kolon  macho yalimiminika machozi kuiona  timu  yao  ikiporomoja  licha  ya  kufanya juhudi  za ziada  kwa  kupata  ushindi  muhimu  jana.

Kolon walihitaji  kupata ushindi  jana  ili  kuweka  hai  matumaini  yao  ya  kubakia  katika daraja  la  kwanza lakini  mabao  ya  haraka  haraka  mnamo  kipindi cha  kwanza ya Breel  Embolo  na  Yevhen Konoplyanka yakiwakatisha  tamaa  , licha  ya  kupigana  kufa  na  kupona  na kukomboa  mabao  hayoMarcel Risse ndie  aliyefunga  bao  la kukomboa  la  FC Kolon  jana.

1. Bundesliga | 1. FC Koeln v FC Schalke 04 (2:2)
Mchezaji wa FC Kolon Dominique Heintz na kocha wake Stefan Ruthenbeck (kulia)Picha: picture-alliance/dpa/F. Gambarini

"Nashukuru  sana , wakati  nikiona , mashabiki wanavyotaka tupambane  tu  kwenda  mbele, licha  ya  kwamba  hisia  zinatuambia hakuna  matumaini na  hata  hivyo  wanaikubali  hali, wakati tumetoka  sare  tu  ya  mabao 2-2 dhidi  ya  Schalke. Pamoja  na hayo inaumiza  sana, kuona  mashabiki  jinsi  walivyovunjika  moyo na  kuumia. Hisia  kama  hizo zinatupata  sisi  kama  wachezaji katika hali  kama  hiyo  uwanjani."

1. Bundesliga | 1. FC Koeln v FC Schalke 04
Wachezaji wa FC Kolon wakipeana pole kwa kushindwa kupata matokeo chanya dhidi ya Schalke 04Picha: picture-alliance/dpa/Revierfoto

Mchezo  wa jana  ulikuwa muhimu  kwa  timu  zote Schalke pamoja na  FC Kolon kwa  kuwa  Schalke ilihitaji  kujiimarisha  katika  nafasi yake  kama  makamu  bingwa  msimu  huu  ikiifuata  Bayern  Munich ambacho  ilikwisha  nyakua  ubingwa  wa  Bundesliga. Schalke  hata hivyo iko na mwanya  wa  pointi pointi  mbili  ikipishana  na  hasimu wake  mkubwa  Borussia  Dortmund  ambayo  ilifanya  maajabu siku ya  Jumamosi  jioni  kwa  kuikandika Bayer Leverkusen kwa  mabao 4-0  katika  mchezo  wa  kwanza  mwaka  huu  kufanya  vizuri  zaidi, kama  anavyosema  kocha  wa  Dortmud Peter Stoeger.

1. Bundesliga 19. Spieltag | Hertha BSC - Borussia Dortmund | Peter Stöger
Kocha wa Borussia Dortmund Peter SoegerPicha: picture-alliance/AP Photo/M. Sohn

"Mpinzani  wetu  alikuwa muhimu, na  tulipata  pointi 3. Inatusaidia, bila  shaka, wengine  wanapaswa kutukimbilia. Lakini  ulikuwa mchezo wa  pointi  muhimu , kwasababu iwapo ungemalizika  kwa sisi  kushindwa , moto  ungewaka, licha  ya  kuwa  tumo  katika eneo  la  nafasi  za  kucheza  katika  Champions League. lakini kungekewa  na  maswali  mengi , kama  ilivyokuwa  huko  nyuma."

Hamburg SV nayo  imo  katika  mchakato  wa  kujinasua  kutoka kushuka  daraja , na  juhudi  hizo  zimezaa  matunda  siku  ya Jumamosi  wakati  walipofanikiwa  kupata  ushindi  mwembamba lakini  muhimu  wa  bao 1-0 dhidi  ya  Freiburg. Hamburg  sasa  ina pointi  25  na  timu iliyoko  juu  yake  tu  ni  Freiburg  yenye  pointi 30.

Hii  ina  maana  timu  hizo  zinapishana  pointi 5 na  kumebakia michezo 3  ligi  kumalizika. Timu 3 zimefungana  katika pointi  30 ambazo  ni VFL Wolfsburg, Mainz 05  na  Freiburg. Katika  michezo mitatu  ijayo  ya  kukunja  jamvi la  Bundesliga , timu  hizo  zitakuwa zinaiangalia Hamburg  kwa  jicho  la  woga  kabla  ya  kumalizika  ligi.

Kama  anavyoelezea  mshambuliaji  wa  Hamburg SV Lewis Holtby.

1. Bundesliga | Hamburger SV - SC Freiburg - Hamburgs Torschütze Lewis Holtby
Lewis Holtby aliyefunga bao la hamburg la ushindi dhidi ya Freiburg akishangilia pamoja na mashabikiPicha: picture-alliance/dpa/C. Charisius

"Wakati  huu, lazima  niseme , najisikia vizuri  sana. Kikosi  kizima, nafikiri, kinajisikia  vizuri. Ulikuwa  ni  ushindi  mihumu  sana leo. Ilikuwa vita, haukuwa  mchezo  rahisi. Lakini  tulitaka  kwa  vyovyote kupata pointi tatu. Hiyo  ilikuwa  muhimu. Tulipaswa  kuonesha sura yetu  ya  mapambano. Tuna michezo mitatu  sasa, wiki  ijayo lijafata mapambano kali ya  wababe  wa  kaskazini. Tunapaswa  kucheza kama  tulivyocheza na kuonesha  kila kitu, ili tuweze kufanikiwa."

Katika  nafasi  ya  kucheza katika  ligi  ya  Ulaya Europa league , TSG Hoffenheim ilisababisha  mazungumzo  ya  kurefusha  mkataba wa  kocha  wa  RB Leipzig Ralph Hasenhuttl  kusitishwa  ghalfa baada  ya  kisago cha  mabao 5-2  nyumbani.

UEFA Europa League Viertelfinale | Olympique Marseille - RB Leipzig | Ralph Hasenhüttl
Kocha wa timu ya RB Leipzig Ralph HasenhuttlPicha: Getty Images/Bongarts/V. Pennicino

VFB Stuttgart imefanikiwa kubakia  katika  daraja  la  kwanza   kwa  kuifunga Werder Bremen kwa  mabao 2-0  kama  ilivyokuwa  kwa  Augsburg ambayo  iliishinda Mainz 05 kwa  mabao 2-0  pia. Werder Bremen na  Hannover 96 bado kimahesabu  hazija jihakikishia  kubakia katika  daraja  la  kwanza  lakini  zimo  katika  nafasi  salama  zaidi.

Mwandishi: Sekione  Kitojo / dpae / afpe / rtre

Mhariri: Yusuf , Saumu