1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

DRC: Makundi ya kijamii yaandamana Beni dhidi ya machafuko

John Kanyunyu DW, Beni27 Novemba 2018

Wazee na viongozi wa madhehebu katika wilaya ya Beni wameandamana kuunga mkono operesheni za pamoja za jeshi la Umoja wa Mataifa na jeshi la Kongo FARDC dhidi ya waasi wa ADF.

https://p.dw.com/p/38yOT
DR Congo Beni
Picha: DW/J. Kanyunyu

Wazee wa busara wa mji wa Beni katika Jamhuri ya Kidemokrasi ya Kongo pamoja na viongozi wa madhehebu mbalimbali wa wilaya ya Beni kwa jumla wameandamana leo, kuunga mkono operesheni za pamoja za jeshi la Umoja wa Mataifa na jeshi la Kongo FARDC dhidi ya waasi wa ADF. Maandamano hayo yanafanyika wakati waasi wa ADF wakiwa wamewauwa raia wawili usiku wa kuamkia leo katika mji mdogo wa Oicha. 

Mwanasheria Nathan Lebabo, msemaji wa waandamanaji, akisoma mbele ya Meya wa mji wa Beni, barua waliyoituma kwa viongozi wa serikali ya Congo pamoja na  wa Umoja wa Mataifa.

Waasi wa ADF hudaiwa kufanya mashambulizi ya mara kwa mara eneo la Beni
Waasi wa ADF hudaiwa kufanya mashambulizi ya mara kwa mara eneo la BeniPicha: DW/J. Kanyunyu

Maandamano haya, yakiwa yanalenga kuwahimiza wanajeshi wa Kongo pamoja na wale wa Umoja huo kupitia kikosi chake maalumu cha kuingilia kati FIB, kuwatokomeza waasi wa Uganda ADF wanaotajwa kuhusika katika mauaji ya raia katika eneo hili kwa kuwakata kwa mapanga.Waandamanaji walitumia fursa hiyo kulaani ukimya wa jumuia ya kimataifa,kuhusu mauwaji ya kila mara katika eneo hili.

Akiwahutubia waandamanaji, baada ya kumkabidhi barua hiyo , Meya wa mji wa Beni Bwanakawa Nyonyi, aliahidi kuituma kwa viongozi wa serikali mjini Kinshasa, na kuwaarifu  wakazi wa Beni wachachokusudia  kukifanya,ili amani ya kudumu iweze kurudi katika mji na wilaya ya Beni .

Naye mwenyekiti wa mashirika ya kiraia katika mji huo Kizito Bin Hangi, akiwa mmoja wa walioandamana, aliiambia DW, kuwa anafurahi kuandamana na wazee wa mji,katika harakati za kusaka amani, na kuyaunga mkono kwa majeshi ya Congo na Monusco.

Waandamanaji walielekea kwenyi ofisi kuu ya Monusco na kumkabidhi pia kiongozi wa kikosi cha Umoja wa Mataifa Monusco, barua ya kuunga mkono operesheni zao.
Waandamanaji walielekea kwenyi ofisi kuu ya Monusco na kumkabidhi pia kiongozi wa kikosi cha Umoja wa Mataifa Monusco, barua ya kuunga mkono operesheni zao.Picha: DW/J. Kanyunyu

Wakati huo huo  Sheikh Aliamin Othman alizipinga kauli  kwamba waislamu wa Bei  wameshindwa kuchukua hatua  ya kuwashawishi waasi wa ADF ambao wengi wao ni waislamu kuacha mauaji ya raia.

Baada ya kumkabidhi Meya barua yao, waandamanaji walielekea kwenyi ofisi kuu ya Monusco katika mji wa Beni, ambako walimkabidhi pia barua hiyo kiongozi wa kikosi cha Umoja wa mataifa Monusco .

Baadaye wataelekea katika kata ya Buili,ambako mi itafanyika ibada kwaajili ya amani itakayoongozwa  na viongozi wa madhehebu mbalimbali .

 

Mhariri: Mohammed Abdul-Rahman