DIYALA:Viongozi wa kisuni wauawa nchini Irak
10 Novemba 2007Matangazo
Mshambuliaji wa kujitoa mhanga aliekuwa amevaa kizibau kilichojaa mabomu ameua viongozi watano wa kisuni katika jimbo la kati la Irak Diyala. Polisi imesema mtu huyo alijilipua wakati wa mkutano wa viongozi wa jimbo hilo.
Waliouawa walikuwa wajumbe wa baraza la ukombozi lilioundwa katika jimbo la Diyala ili kupambana na al-kaida katika sehemu hiyo.