Dawa mpya ya watoto ya kupambana na makali ya HIV sasa imewasili Kenya. Dolutergravir inaaminika kuwa silaha muhimu kwenye vita dhidi ya maambukizi ya HIV kwani ina ladha ya stroberi na inaweza kuchanganywa na chakula au maziwa. Kadhalika uwezekano wa kuwa sugu mwilini ni mgodo pamoja na athari zake.