Aleva Ndavogo Jude ndiye kiongozi wa 'Tchado Stars', kundi la vijana kutoka mji mkuu wa Chad N’Djamena. Amekuwa akicheza kila siku na watoto wa mitaani kwa mwaka moja na nusu sasa. Kutoka wazo la hiari, ilitokea kazi kubwa. Hivi sasa anawahudumia wavulana kati ya 30 na 40 wenye umri kuanzia miaka 8 hadi 28, na anajaribu kuwarudisha kwa familia zao au kuwatafutia kazi ili waishi maisha bora.