1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Chama tawala Chad chashinda wingi wa viti bungeni

Sylvia Mwehozi
12 Januari 2025

Chama tawala nchini Chad kimeshinda theluthi mbili ya viti katika uchaguzi wa wabunge uliofanyika mwezi uliopita kulingana na matokeo ya muda yaliyotolewa Jumapili.

https://p.dw.com/p/4p4uY
Mahamat Deby Itno / Chad
Wanajeshi wakipita kando ya bango la uchaguzi la Mahamat Idriss Deby Picha: Issouf Sanogo/AFP/Getty Images

Chama tawala nchini Chad kimeshinda theluthi mbili ya viti katika uchaguzi wa wabungeuliofanyika mwezi uliopita kulingana na matokeo ya muda yaliyotolewa leo. Matokeo ya uchaguzi huo ambao kwa kiasi kikubwa ulisusiwa na upinzani, yanaimarisha utawala wa Rais Mahamat Idriss Deby madarakani.

Mamlaka ya uchaguzi imetangaza kuwa chama cha Deby cha Patriotic Salvation Movement, kimejizolea jumla ya viti 124 kati ya 188 katika bunge la kitaifa.

Uchaguzi huo ambao ulijumuisha chaguzi za manispaa na mikoa, ulisusiwa na chama cha kiongozi wa upinzani Succes Masra pamoja na vyama vingine kadha, vikisema ulikosa uwazi.

Deby alishinda urais katika uchaguzi mwingine iliozozaniwa mwezi Mei, miaka mitatu baada ya kujitangaza kuwa kiongozi wa muda wakati waasi walipomuua baba yake kwenye uwanja wa vita.