BERLIN:Uchumi kustawi kwa asilimia 2.2 katika mwaka ujao
18 Oktoba 2007Matangazo
Wataalam wa uchumi wametoa mwito kwa kansela wa Ujerumani Angela Merkel juu ya kusonga mbele na mageuzi kwa mwendo wa kasi zaidi.
Wataalamu hao wametoa mwito huo katika ripoti juu ya uchumi wa Ujerumani unaotabiriwa kuwa ustawi utafikia asilimia 2.2 katika mwaka ujao badala ya asilimia 2.4.
Hata hivyo wamesema ustawi katika mwaka huu utafikia asilimia 2.6 kadhalika wametabiri kwa mara ya kwanza baada ya miaka mingi kwamba Ujerumani itakuwa na bajeti itakayofikia ziada.