1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

BERLIN:Bunge la Ujerumani laidhinisha bajeti ya mwaka 2008

4 Julai 2007
https://p.dw.com/p/CBlv

Bunge la Ujerumani limeidhinisha bajeti ya mwaka 2008 iliyowasilishwa na waziri wa fedha Peer Steinbrück.

Kwa mujibu wa msemaji wa serikali mswaada huo wa bajeti unajumuisha mkopo wa kiasi cha euro billioni 13.

Kiasi hicho ni kidogo kabisa katika bajeti ikilinganishwa na miaka iliyopita. Kulingana na muswaada huo ujerumani imepania kupunguza matumizi yake hadi kusawazisha bajeti ifikiapo mwaka 2011.