1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

BERLIN : Mahkama yatafakari uchunguzi wa mawasiliano

10 Oktoba 2007
https://p.dw.com/p/C7Gw

Mahkama Kuu nchini Ujerumani inatazamiwa kuanza kusikiliza hoja kwa kiasi gani taifa linaweza kurekodi mazungumzo ya simu na kuchunguza mawasiliano ya mtandao katika juhudi za kuzuwiya ugaidi.

Suala linalojadiliwa ni sheria katika mkoa wa North Rhine Westphalia ambayo inaruhusu polisi kufanya upekuzi wa mtandao bila ya vibali vya upekuzi.

Watetezi wa suala la faragha nchini Ujerumani wanapinga hatua hizo kwa kusema kwamba ni kinyume na katiba kwa kuwa kutapelekea kupelelezwa kwa watu wa kawai