Benitez ndiye kocha mpya wa Newcastle
11 Machi 2016Matangazo
Benitez mwenye umri wa miaka 55, kocha wa zamani wa Liverpool na Real Madrid, ana michuano kumi pekee kuidumisha hadhi ya Newcastle katika Premier League huku moja ya michuano hiyo ikiwa dhidi ya viongozi wa ligi Leicester City Jumatatu ijayo.
Taarifa ya Newcastle imesema Benitez ambaye alishinda Kombe la Europa akiwa kaimu kocha wa Chelsea, amesaini mkataba wa awali wa miaka mitatu. Amewaleta makocha wasaidizi Fabio Pecchia, Francisco de Miguel Moreno na Antonio Gomez Perez.
Mwandishi: Bruce Amani/AFP/DPA/AP
Mhariri: Gakuba Daniel