BEIRUT: Jeshi laendelea na operesheni ya kuwangóa wanamgambo
23 Juni 2007Matangazo
Jeshi la Lebanon limesema,linaendelea na operesheni za kijeshi katika kambi ya wakimbizi wa Kipalestina ya Nahr al-Bared,kaskazini mwa Lebanon.Lengo la operesheni hiyo ni kuwangóa wapiganaji wa kundi la Fatah al-Islam waliobakia katika kambi hiyo.Hapo awali,waziri wa ulinzi wa Lebanon alisema,wanamgambo hao wa Kiislamu waliojificha kambini wameshindwa,na sasa jeshi linashughulika na operesheni ya kuisafisha kambi hiyo.