Beijing:Vigogo watatu China wastaafu kamati kuu ya chama
21 Oktoba 2007Matangazo
Wanasiasa watatu wa ngazi ya juu nchini China wanastaafu, akiwemo Makamu wa Rais Zeng Qinghong. Wengine ni Wu Guanzheng mkuu wa tume ya kupambana na rushwa, na Luo Gan anayesimamia idara ya polisi na usalama nchini humo. Kustafu kwao kumetangwa katika siku ya mwisho ya mkutano mkuu wa siku tano wa chama tawala cha kikoministi. Kesho mkutano huo unatarajiwa kumuidhinisha rais Hu Jintao kuendelea kuwa kiongozi wa chama kwa miaka mitano ijayo pamioja na kuichagua kamati kuu ya watu 9, chombo kinachotawala nchini humo.