BEIJING:19 wafa katika mlipuko kwenye mgodi wa makaa ya mawe
29 Machi 2007Matangazo
Kumetokea mlipuko wa gesi kwenye mgodi mmoja wa makaa ya mawe huko China ambapo wachimbaji 19 wameuawa na wengine 9 hawajulikani walipo.
Shirika la habari la China limearifu kuwa , tukio hilo limetokea katika mgodi wa Linfei katika jimbo la Shanxi, ikiwa ni siku 10 tu baada ya tukio lingine kama hilo, lililopelekea vifo vya wachimbaji 21.
Migodi ya makaa ya mawe nchini China ni migodi hatari duniani, ikiwa na matukio ya kila siku, ya milipuko na mafuriko, pamoja na serikali ya nchi hiyo kuahidi kuboresha hali hiyo.