1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

BARCELONA: Washukiwa ugaidi wamekamatwa Hispania

27 Juni 2007
https://p.dw.com/p/CBo1

Wanaume 3 wanaotuhumiwa kuajiri watu watakaoweza kutumiwa kama magaidi kwa niaba ya mtandao wa al-Qaeda,wamekamatwa nchini Hispania.Polisi imesema, wanaume hao watatu walikamatwa mjini Barcelona na wanahusika na kundi linaloitwa,“Shirikisho la al-Qaeda katika eneo la Kiislamu la Maghreb“.Hivi karibuni,maafisa wa Ulaya wanaopambana na ugaidi, walionya kwamba chama kilichokuwa na makao yake nchini Algeria,kinajaribu kueneza harakati zake barani Ulaya.