1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

BAGHDAD: Wabunge wafuasi wa Moqtada al-Sadr kurejea bungeni

21 Januari 2007
https://p.dw.com/p/CCZ2
Waziri wa nje Rice(katikati) na Waziri wa ulinzi Gates(kushoto) wakikutana na Rais Hosni Mubarak wa Misri(kulia) katika mji wa pwani Sharm-el-Sheikh nchini Misri
Waziri wa nje Rice(katikati) na Waziri wa ulinzi Gates(kushoto) wakikutana na Rais Hosni Mubarak wa Misri(kulia) katika mji wa pwani Sharm-el-Sheikh nchini MisriPicha: AP

Kundi la wabunge wafuasi wa kiongozi wa Kishia Moqtada al-Sadr nchini Iraq limekubali kurejea bungeni baada ya kulisusia bunge hilo kwa muda wa miezi miwili.

Kundi hilo ni mshirika muhimu wa Waziri Mkuu wa Iraq, Nouri al-Maliki, lakini limekuwa likisusia vikao vya bunge tangu mwezi Novemba mwaka uliopita likitaka majeshi ya Marekani kuondoka nchini humo.

Kundi hilo pia lilisusia bunge kupinga mkutano uliofanyika kati ya Nouri al-Maliki na Rais wa Marekani, George W. Bush..

Marekani inalichukulia kundi la wanamgambo la Mahdi linaloongozwa na Moqtada al-Sadir kuwa tishio kubwa la usalama nchini Iraq.