1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Baghdad. Nouri al-Maliki awashutumu Wasunni .

13 Desemba 2006
https://p.dw.com/p/CCjm

Waziri mkuu wa Iraq Nouri al-Maliki amewalaumu wasunni wenye msimamo mkali na wale wanaomuunga mkono dikteta wa zamani Saddam Hussein kwa shambulio baya kabisa la bomu dhidi ya soko moja mjini Baghdad jana asubuhi.

Zaidi ya watu 70 , wengi wao wakiwa masikini kutoka katika jamii ya Washia wameuwawa wakati mshambuliaji wa kujitoa muhanga alipolipua gari lake katika kundi la wafanyakazi vibarua wanaotafuta ajira katika mji huo.

Zaidi ya watu 200 wamejeruhiwa.

Iraq imekumbwa na machafuko ya kimadhehebu baina ya Washia na Wasunni kwa muda mwingi wa mwaka huu. Kutokana na machafuko hayo, rais wa Marekani George W. Bush anatarajiwa kupitia upya sera za utawala wake nchini Iraq mapema mwaka ujao.