1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Arsenal yataka kuonyesha maajabu

13 Machi 2013

Uzoefu wa klabu ya Arsenal ya Uingereza katika michuano ya Champions League pamoja na nia waliyonayo,inatoa kwa timu hiyo haki ya kuamini kuwa wanaweza kubadilisha matokeo ya kufungwa mabao 3-1 nyumbani na FC Bayern.

https://p.dw.com/p/17wFi
epa03591222 Lukas Podolski of Arsenal (2nd L) scores the 1-2 against Bayern Munich during the UEFA Champions League match between Arsenal and Bayern Munich at the Emirates Stadium in London, Britain, 19 February 2013. EPA/KERIM OKTEN +++(c) dpa - Bildfunk+++
Arsenal FC ilipopambana na BayernPicha: picture-alliance/dpa

Wakati timu hizo zitakapokutana tena leo jioni(13.03.2013) katika mchezo wa mwisho wa kuamua nani ataingia katika robo fainali. Hii ni kwa mujibu wa kocha wa timu hiyo Aserne Wenger. Mchezo mwingine ni kati ya Porto ya Ureno dhidi ya Malaga ya Uhispania.

Arsenal inaonekana kuwa timu ya tatu katika historia ya mashindano hayo , kufungwa nyumbani katika duru ya mtoano lakini hatimaye kuweza kushinda ugenini na kusonga mbele.

Wachezaji kadha wa Arsenal hata hivyo hawatakuwamo katika kikosi hicho , nao ni pamoja na Jack Wilshere, Lukas Podolski na Bacary Sagna, na hali hii imeufanya mzigo mzito unaokabili timu hiyo mbele ya Bayern kuwa mkubwa zaidi , lakini Wenger amesema timu yake iko tayari kufanya maajabu makubwa.

Montpellier's French midfielder Jamel Saihi, left, challenges for the ball with Arsenal's German forward Lukas Podolski, during the Champions League Group B soccer match between Montpellier and Arsenal, at the La Mosson stadium, in Montpellier, southern France, Tuesday, Sept.18, 2012. (AP Photo/Claude Paris)
Lukas Podolski hatakuwapo kupambana na BayernPicha: AP

Mtaduwaa

"Ni matumaini yangu kuwa tutamshangaza kila mtu leo jioni," amesema Wenger huku akitabasamu wakati akizungumza na waandishi habari. "Ndio tunamajeruhi lakini tumekuja hapa na kikosi kizuri ambayo ina motisha.

"Kitu muhimu ni kuingia katika mchezo huu kwa kuweka mbinyo haraka na kupata goli la mapema. Imani yetu haijaweza kujaribiwa kama itakavyokuwa jioni ya leo, amesema kocha huyo raia wa Ufaransa.

Wenger ambaye amemuacha nyumbani London mlinda mlango namba moja wa timu hiyo Wojciech Szczesny akisema mchezaji huyo amechoka kiakili baada ya msimu mrefu , amesema kuwa timu yake itahitaji kupata uwiano sahihi baina ya nia halisi na uhuru uwanjani kutokana na matokeo ya awali katika mchezo wa kwanza.

"Ni hali ngumu, ndio lakini kwamba haiwezekani , hapana, amedokeza Wenger.

Kocha wa Bayern Munich Jupp Heynckes amewaonya wachezaji wake watarajie kisichotarajiwa kutoka kwa kikosi cha Wenger.

ARCHIV - Trainer Jupp Heynckes vom FC Bayern München lächelt am 01.12.2012 in München (Bayern). 1000 Mal Bundesliga - das hatte sich Jupp Heynckes beim Debüt als 20 Jahre junger Spieler nicht ausgemalt. Die Partie gegen Bremen mit dem «kleinen Jubilar» Schaaf (750. Partie) ist für die Bayern vor allem aber eine Art Warm-up für das Pokalduell mit Dortmund. Foto: Marc Müller/dpa (zu dpa-Korr.: "«Imposante Zahl»: Heynckes macht 1000 voll - Warm-up für Robben« vom 22.02.2013) +++(c) dpa - Bildfunk+++
Kocha Jupp Heynckes wa FC Bayern MünchenPicha: picture-alliance/dpa

Henckes awatahadharisha Bayern

"Tunapaswa kuwa waangalifu , hata kama tumeshinda mchezo wa kwanza kwa mabao 3-1.

"Mafanikio yamekuja kwa Arsenal wakati Arsene alipowasili katika timu hiyo.

"Kwa muda wa miaka mingi walicheza soka nzuri sana nchini Uingereza, kama sio kila mara timu iliyopata mafanikio makubwa.

Wakati huo huo Sir Bobby Charlton mchezaji wa zamani wa kikosi cha Uingereza kilichonyakua ubingwa wa dunia kwa mara ya kwanza na ya mwisho hadi sasa , ameashiria kuwa Bayern Munich inaweza kutoroka na taji la Champions League msimu huu.

Bayern yaweza kunyakua taji: Chalton

Iwapo natakiwa kutaja timu moja , naweza kuitaja Bayern Munich kushinda Champions League, amesema mchezaji huyo wa zamani mwenye umri wa miaka 75.

Mchezaji huyo wa zamani wa Manchester United , ambaye alikuwamo katika kikosi kilichonyakua ubingwa wa dunia mwaka 1966, amesema mahasimu wa Bayern Munich katika Bundesliga , Borussia Dortmund nayo pia inaweza kufika katika fainali ya Champions League katika uwanja wa Wembley hapo Mei 25.

Borussia Dortmund's Felipe Santana (3rd L) celebrates his goal against Shakhtar Donetsk during their Champions League soccer match in Dortmund March 5, 2013. REUTERS/Wolfgang Rattay (GERMANY - Tags: SPORT SOCCER)
Borussia DortmundPicha: Reuters

Schalke 04 walibaki midomo wazi jana wakitafakari kilichowapata hadi kuondolewa tonge mdomoni baada ya kubandikwa mabao 3-2 nyumbani dhidi ya Galatasaray ya Uturuki. Baada ya sare ya bao 1-1 ugenini , Schalke ilikuwa inaonekana kurejea katika robo fainali kwa mara ya tatu kufuatia kufanya hivyo mwaka 2008 na 2011. Lakini Schalke waliporomoka kwa kipigo cha mabao 2-1 hadi mapumziko baada ya mabao mawili katika dakika nane za mwisho wa kipindi cha kwanza "Inauma , Tulicheza vizuri katika michezo yote. "Tumetolewa bila sababu,"

amesema mlinda mlango wa Schalke Timo Hildebrand.

Nayo Barcelona ilito cheche jana baada ya kufuta mabao 2-0 ya AC Milan yaliyopatikana katika mchezo wa kwanza na kupachika mabao 4-0 jana. AC Milan haikuonekana kuwa na jibu lolote katika mchezo huo ambao Lionel Messi alionyesha kuwa yeye ni moto wa kuotea kwa mbali.

Messi binadamu wa ajabu

Gary Lineker mchezaji wa zamani wa Barca na Uingereza ambaye hivi sasa ni mchambuzi wa masuala ya soka , amesema katika ukurasa wake wa Twitter, "Nimefurahi Barca imefanikiwa kusonga mbele. Ulikuwa ni ushindi dhidi ya kila kipingamizi na ushindi kwa mchezo wa mpira.

epa03170119 Argentinian striker Lionel 'Leo' Messi of FC Barcelona celebrates after scoring his team's 1-0 by penalty during their UEFA Champions League quarterfinal return match at the Camp Nou stadium in Barcelona, north-eastern Spain, on 03 April 2012. EPA/ANDREU DALMAU +++(c) dpa - Bildfunk+++
Lionel Messi wa BarcelonaPicha: picture-alliance/dpa

Marco Materazzi, mlinzi wa zamani wa Inter Milan na Italia, katika Twitter, amesema Habemus Messi ! Wamemuumba kutoka wapi kiumbe huyu wa ajabu? Huyu si binadamu.

Gazeti la Marca la Hispania : Leo, shujaa tena. Messi amejibu wale waliokuwa wakimtilia shaka kwa kuonyesha mchezo wa ajabu.

Mwandishi: Sekione Kitojo / rtre / afpe

Mhariri: Mohammed Khelef