1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Aliyekuwa nahodha wa Man United Vidic astaafu

29 Januari 2016

Aliyekuwa beki wa klabu ya Manchester United ya England, Nemanja Vidic ametangaza kustaafu kutoka kandanda akiwa na umri wa miaka 34

https://p.dw.com/p/1Hm11
Champions League Manchester United - Bayern München
Picha: Getty Images/Alex Livesey

Vidic alishinda mataji matano ya Premier League na Kombe la Mabingwa Ulaya mwaka wa 2007-2008 wakati wa miaka yake minane uwanjani Old Trafford, lakini akakumbwa na majeraha yaliyomlazimu kuamua kuzitundika njumu.

Mserbia huyo aliruhusiwa kuondoka klabu yake ya Inter Milan mapema mwezi huu baada ya kipindi cha miezi 18 nchini Italia iliyojaa majeraha. Vidic alijiunga na United akitokea Spartak Moscow mnamo Januari 2006 na akaweka ushirikiano imara katika safu ya ulinzi na Rio Ferdinand.

Mwandishi: Bruce Amani/AFP/AP/DPA/reuters
Mhariri: Daniel Gakuba