Wakati zoezi la kuhesabu kura likiendelea nchini kote Tanzania Bara na Visiwani, Chama cha Mapinduzi CCM kimeendelea kujikusanyia kura kwa nafasi ya Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kuwaacha mbali washidani wake takribani 14 huku kikiendelea kushinda viti zaidi vya Ubunge,huku chama kikuu cha Upinzani Chadema kikipoteza kwa kasi viti vya ubunge na uimara wake nchini Tanzania.