Wakati operesheni za pamoja kati ya majeshi ya Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo na yale ya Umoja wa mataifa Monusco dhidi ya lundi la waasi la Allied Democratic Forces-ADF zinaendelea katika viunga vya mji wa Beni, raia wa vijiji vya Ngite, Mangboko, Mbau,Oicha,Mukoko na Kokola kaskazini mwa mji wa Beni, wanaishi katika hali ya wasiwasi wakitegemea mashambukizi ya ADF.