Katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, upinzani, tume huru ya uchaguzi na serikali zimetupiana lawama kufuatia kuungua kwa ghala ya vifaa vya uchaguzi zikiwemo mashine za kupigia kura hapo jana// Bunge la Umoja wa Ulaya limeorodhesha matukio kadhaa yanayokiukwa nchini Tanzania na limeitolea wito serikali ya Tanzania kurekebisha mwenendo wake na kuacha kukiuka haki za binaadamu.