Zanzibar imesherehekea miaka 54 tangu mapinduzi ya tarehe 12.01.1964. Sherehe hizo zilizofanyika mjini Zanzibar zimeongozwa na rais wa Zanzibar Ali Mohammed Shein, na zimehudhuriwa na viongozi wa pande mbili za muungano wa Tanzania, akiwemo Rais John Magufuli. Katika hotuba yake Rais Shein amesema serikali yake inachukuwa hatua za kuimarisha uchumi kama vile utalii, na kuboresha zao la karafuu.