1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Watu 30 wafamaji Uganda

Isaac Gamba
27 Desemba 2016

Karibu watu 30 wamekufa maji baada ya boti ya abiria iliyokuwa imejaa kupitiliza kiasi kuzama katika Ziwa Albert, magharibi mwa Uganda.

https://p.dw.com/p/2UuYC
Uganda Schiffsunglück Lake Albert
Picha: Getty Images/AFP/M. Siiloni

Polisi wa Uganda wameripoti kuwa boti hiyo ilikuwa imewabeba watu 45. Wameongeza kuwa watu 21 hawajulikani walipo, wakati miili tisa ikiokolewa. Wengine 15 waliokolewa na wavuvi pamoja na polisi. Ajali za majini ni jambo la kawaida nchini Uganda, kwa sababu vyombo vingi vya majini vimekuwa vikitengenezwa ndani bila ya kuwapo na vifaa vya uokoaji.