1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Watu 19 wauawa katika mkanyagano

25 Julai 2010

Watu 19 wamepoteza maisha yao kwenye mkanyagano uliotokea wakati wa tamasha la muziki Love Parade mjini Duisburg, Ujerumani. Zaidi ya watu 340 wamejeruhiwa.

https://p.dw.com/p/OUAD
Hilfskraefte versorgen am Samstag, 24. Juli 2010, in Duisburg, Nordrhein-Westfalen, beim Techno-Musikfestival Loveparade 2010 nach einer Panik kollabierte Teilnehmer. Vor dem Gelaende vor der Loveparade in Duisburg ist es am Samstag zu einer Massenpanik gekommen. Nach Angaben der Polizei wurden dabei zehn Menschen getoetet. (apn Photo/Hermann J. Knippertz) --- Collapsed people get first aid after a panic on this year's techno-music festival "Loveparade 2010" in Duisburg, Germany, on Saturday, July 24, 2010. (apn Photo/Hermann J. Knippertz)
Majeruhi wakipata matibabu mbele ya ujia unaoelekea kwenye uwanja wa tamasha la muziki "Love Parade."Picha: AP

Mkanyagano huo ulitokea kwenye ujia mwembamba kuelekea kwenye uwanja wa tamasha. Hadi sasa haijulikana kilichosababisha kuzuka kwa mkanyagano huo.

Kuna mashahidi wanaosema kuwa watu walibanana katika ujia huo na wengine waliojaribu kuparamia ukuta na ngazi waliporomoka. Waandalizi wa tamasha hilo wanazidi kukosolewa. Zaidi ya watu milioni moja walihudhuria tamasha hilo katika eneo lenye uwezo wa kuchukua robo ya idadi hiyo.

Maafa hayo yamesababisha huzuni na mshtuko mkubwa miongoni mwa umma hapa Ujerumani na katika nchi za nje. Rais wa Ujerumani Christian Wulff amesema fikra zake zipo kwa wahanga wa ajali hiyo,familia zao na marafiki zao. Vile vile ametoa mwito wa kufanywa uchunguzi wa kina kuhusu maafa hayo. Kansela wa Ujerumani Angela Merkel na mwenyekiti wa chama cha SPD Sigmar Gabriel pia wametoa pole kwa familia za wahanga.

Waziri Mkuu wa jimbo la North Rhine Westphalia, Hannelore Kraft akiwa katika hali ya huzuni alitoa rambirambi kwa familia za wahanga na amesema, wale waliojeruhiwa watashughulikiwa ipasavyo. Halikadhalika Rais wa Kamisheni ya Umoja wa Ulaya, José Manuel Barroso ametoa rambirambi zake kwa familia zilizofiwa kutokana na mkanyagano uliotokea katika tamasha la muziki "Love Parade" nchini Ujerumani.

Mwandishi: P.Martin/dpa

Mhariri: M.Dahman