Watoto Geita walazimika kuchagua kati ya chakula na masomo
Hawa Bihoga13 Aprili 2016
Ingawa serikali ya Tanzania inataka kutoa elimu kwa kila mtoto, baadhi ya watoto wa mkoani Geita wamesema wanapendelea kufanya kazi migodini au kuvua samaki kwani familia zao hazina pesa ya kutosha na hawataki kulala njaa. Hawa Bihoga amewatembelea na kushuhudia hali ya maisha yao.