1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

WASHINGTON: Usalama wa Iraq kujadiliwa ana kwa ana

18 Mei 2007
https://p.dw.com/p/CC14

Marekani na Iran zinataka kuzungumza ana kwa ana tarehe 28 mwezi huu.Majadiliano hayo yatahusika na hali ya usalama nchini Iraq.Mkutano huo unatazamiwa kufanywa mjini Baghdad.Hayo yatakuwa majadiliano ya kwanza ya ngazi ya juu kupata kufanywa kati ya pande hizo mbili,tangu miaka kadhaa.Serikali ya Washington inaituhumu Teheran kuwa inawasaidia wanamgambo wa madhehebu ya Kishia nchini Iraq,lakini Iran inakanusha lawama hizo.