1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Viongozi wa Ulaya watoa mwito machafuko nchini Kenya yakomeshwe

30 Januari 2008
https://p.dw.com/p/CzXc

Viongozi watano wa Ulaya wametoa mwito machafuko yanayoendelea nchini Kenya yakomeshwe wakisema ipo haja ya viongozi wa nchi hiyo kuzungumza kwa masilahi ya taifa na eneo zima kwa jumla.

Katika taarifa yao ya pamoja viongozi wa Uingereza, Ufaransa, Ujerumani, Italia na halmashauri ya Umoja wa Ulaya, wamewataka wanasiasa wa Kenya wachukue hatua za dharura kumaliza ghasia na kurejesha usalama kwa wakenya wote.

Taarifa hiyo iliyotolewa baada ya mkutano ulioandaliwa na waziri mkuu wa Uingereza, Gordon Brown mjini London, ambao ulijadili matatizo ya kiuchumi duniani, pia imesema viongozi hao wanaziunga mkono juhudi za katibu mkuu wa zamani wa Umoja wa Mataifa, Kofi Annan, rais mstaafu wa Tanzania, Benjamin Mkapa na Graca Machel, mke wa rais wa zamani wa Afrika Kusini, Nelson Mandela.