Mahakama mkoani Lindi, Tanzania imewahukumu viongozi wawili wa chama cha CHADEMA kwenda jela miezi minane, ikiwa ni pamoja na mwenyekiti wa chama hicho Mkoani Lindi Suleiman Methew. Wiki iliyopita mbunge mwingine wa chama hicho alihukumiwa kifungo cha miezi sita gerezani. Mchambuzi wa masuala ya kisheria nchini Tanzania, Hussein Sengu, anaelezea mtazamo wa kisheria kuhusiana na hukumu hizo.