1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Viongozi wa Afrika walaumiwa

Grace Kabogo
4 Septemba 2017

Wajumbe kutoka bara la Ulaya na Afrika wamewalaumu viongozi wa mabara hayo kwa kuchukulia uhamiaji kuwa suala la uhalifu bila kutilia maanani sababu za watu hasa vijana kuhatarisha maisha yao kwenda nchi nyengine.

https://p.dw.com/p/2jJsf

Kwenye kongamano la siku tatu lililoanza hapo jana mjini Kampala, Uganda, vijana wakimbizi na wahamiaji walisimulia madhila yao wakielezea kuwa jamii ya kimataifa inatakiwa kurahisisha uhamiaji pamoja na kushinikiza serikali za Afrika kuzingatia utawala bora ili kuondoa wazo kwamba nyumbani si salama, ila tu mtu akikimbilia nchi nyingine.

Ungana na mwandishi wetu Lubega Emmanuel kutoka Kampala katika taarifa hii.