1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Uswisi yazuia mali za Ben Ali

Kabogo Grace Patricia20 Januari 2011

Serikali ya Shirikisho la Uswisi imezuia mali za rais aliyeondolewa madarakani nchini Tunisia, Zine El Abidine Ben Ali na familia yake zilizoko nchini Uswisi.

https://p.dw.com/p/zzrG
Waziri wa Mambo ya Nje wa Uswisi, Micheline Calmy-ReyPicha: AP

Waziri wa Mambo ya Nje wa Uswisi, Micheline Calmy-Rey amesema anataka kuzuia matumizi yoyote mabaya ya fedha za umma.

Wakati huo huo, Benki Kuu ya Tunisia imeichukua taasisi ya kifedha iliyokuwa inadhibitiwa na mkwe wa Ben Ali.

Mapema, viongozi wa Tunisia walisema pia watachunguza mali za Ben Ali zilizopo nje ya nchi zikiwemo akaunti za benki na nyumba.

Zine El Abidine Ben Ali
Rais aliyeondolewa madarakani Tunisia, Zine El Abidine Ben AliPicha: picture alliance / dpa

Imeripotiwa kuwa Ben Ali aliyekimbilia Saudi Arabia Ijumaa iliyopita aliondoka nchini Tunisia na tani 1.5 za madini ya dhahabu.

Kwa upande mwingine, karibu waandamanaji 2,000 katika mji mkuu wa Tunis wanadai kufukuzwa kwa mawaziri wote ambao wanahusishwa na Ben Ali katika serikali mpya ya muungano.

Na taarifa nyingine zinaeleza kuwa viongozi wa serikali hiyo ya mpito wamewaachilia huru wafungwa wa mwisho wa kisiasa.