1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Ujerumani yazindua kikosi cha mwisho

2 Juni 2016

Kocha wa timu ya taifa ya Ujerumani Joachim Löw amekitangaza kikosi chake cha mwisho cha wachezaji 23 watakaoelekea Ufaransa kucheza katika dimba la Kombe la Mataifa ya Ulaya - Euro 2016

https://p.dw.com/p/1Iykt
Benedikt Hoewedes DFB PK Pressekonferenz Sami Khedira Jogi Löw
Picha: picture-alliance/dpa/M. Gilliar

Orodha hiyo imekosa jina la mshambuliaji wa Borussia Dortmund Marco Reus, ambaye ameachwa nje kwa sababu za kiafya. Aidha Löw amewatema wachezaji wawili wa Bayer Leverkusen Karim Bellarabi na Julian Brandt. Sebastian Rudy wa Hoffenheim pia hatocheza katika Euro 2016.

Kikosi kamili:

Makipa: Manuel Neuer (Bayern Munich), Marc-Andre ter Stegen (Barcelona), Bernd Leno (Bayer Leverkusen).

Mabeki: Jonas Hector (Cologne), Benedikt Höwedes (Schalke), Shkodran Mustafi (Valencia), Antonio Rüdiger (Roma), Emre Can (Liverpool), Jerome Boateng (Bayern Munich), Mats Hummels (Borussia Dortmund)

Viungo: Sami Khedira (Juventus), Toni Kroos (Real Madrid), Mesut Özil (Arsenal), Andre Schürrle and Julian Draxler (both Wolfsburg), Thomas Müller and Joshua Kimmich (both Bayern Munich), Julian Weigl (Borussia Dortmund), Lukas Podolski (Galatasaray), Bastian Schweinsteiger (Manchester United).

Washambuliaji: Mario Götze (Bayern Munich), Mario Gomez (Besiktas), Leroy Sane (Schalke)

Mwandishi: Bruce Amani/DW
Mhariri: Sekione Kitojo