1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Ujerumani yawasili Urusi tayari kwa kombe la dunia

Admin.WagnerD12 Juni 2018

Mabingwa watetezi wa kombe la dunia Ujerumani wamewasili Urusi majira ya saa saba mchana na kujiunga na hafla kubwa  ya kombe la dunia wakati Ubelgiji ikichukulia bila kujali hofu ya kuumia kwa nyota wake Eden Hazard

https://p.dw.com/p/2zOGq
Fußball WM 2018 Mannschaftsfoto DFB Nationalteam Deutsche Nationalmannschaft
Picha: Imago/Revierfoto

Kikosi  cha  vijana  chipukizi  wa  England  kinachoongozwa  na kocha Gareth  Southgate  pia  kilitarajiwa  kuwasili  leo  wakati shauku  ikiongezeka  kabla  ya  ufunguzi  rasmi  wa  fainali  hizo hapo  Alhamis mjini  Moscow  kati  ya  wenyeji  wa  mashindano hayo  Urusi   dhidi  ya  saudi  Arabia.

England Training und Pressekonferenz - Tottenham Hotspur Football Club Trainingsgelände
Kocha wa timu ya taifa ya Gareth SouthgatePicha: picture-alliance/D.Klein

Lakini kabla  ya  shughuli  hiyo  kuanza  uwanjani , wanachama  wa shirikisho  la  kandanda  duniani  FIFA  watakuwa  na  kibarua  cha kuchagua  iwapo  wayazawadie  mataifa ya  Amerika  ya  kaskazini ama  Morocco  uenyeji  wa  michuano  ya  fainali  za  mwaka  2026.

Ujerumani , ambayo iliiangusha  Argentina  katika  fainali  nchini Brazil  miaka  minne  iliyopita , inalenga  kujiunga  na  Brazil  kama washindi  mara  tano  wa  taji  hilo lakini  kuna  maswali  kuhusiana na  jinsi  wanavyocheza  kwa  sasa   wakati  wakiingia  katika mashindano  haya.

Kikosi  cha  Joachim Loew  kimecheza  michezo  mitano   bila  ya kushinda  kabla  ya  kufanyakazi  ya  ziada  na  kuishinda  Saudi Arabia  kwa  mabao  2-1  katika  mchezo  wao  wa  mwisho  wa kujiweka  tayari  na  mlinda  mlango  namba  moja  Manuel Neuer haja  cheza katika  ligi  tangu  Septemba  mwaka  jana.

WM 2018 - Trainingslager Deutschland - Pressekonferenz
Kocha wa timu ya taifa ya Ujerumani Joachim LoewPicha: picture alliance / Christian Charisius/dpa

Wajerumani  hufika  angalau nusu  fainali

Lakini  Wajerumani  wamefika  angalau katika  nusu  fainali  katika fainali  nne  za  kombe  la  dunia   na  timu  hiyo  ina  tabia  ya kuanza  kucheza  vizuri  wakati  wanahitaji  kufanya  hivyo  sana.

Mabingwa  hao  watetezi  wanaaza  kampeni  yao  ya  kombe  la dunia  dhidi  ya  Mexico  Juni 17  mjini  Moscow.   Pia  wanacheza dhidi  ya  Sweden ba  Korea  kusini  katika  kundi  F.

Ujerumani  haiendi  Urusi  kutalii, "lakini  kushinda  mashindano hayo," amesema  mkurugenzi  wa  timu  hiyo Oliver Bierhoff.

England  sio  miongoni mwa  timu  zinazopigiwa  upatu  kutoroka  na kombe  hilo  nchini  Urusi  lakini  kikosi  hicho  cha   tatu  cha  vijana chipukizi  kinachokwenda   na  chapa  ya  Simba  watatu  kinaingia katika  kinyang'anyiro  hicho  cha  kombe  la  dunia  kikijivunia  nyota wa  ligi  ya  England  ya  Premier League  Harry Kane, Dele  Alli  na Raheem Sterling.

EM Qualifikation England gegen Litauen am 27.03.2015
Mshambuliaji chipukizi Raheem Sterling wa Uingereza akivaa jezi namba 7Picha: Ian Walton/Getty Images

Tuna timu  ya  vijana  wadogo  lakini  wenye  uchu  ambao  wanataka kufika  mbali , tunataka  kuileta  nchi  yetu  pamoja  na kufanikisha kitu  kikubwa,"  alisema  Alli.

Wapinzani  wa  Uingereza  katika  kundi G  Ubelgiji  walionesha vipaji  vyao   katika  ushindi  wa  mabao 4-1 dhidi  ya  Costa Rica mjini  Brussels  siku  ya  Jumatatu,  ikiwa  ni  pamoja  na  mabao mawili  kutoka  kwa  mshambuliaji  wa  Manchester United Romelu Lukaku  na  nyota  wao  Hazard  kutoka  Chelsea.

Hazard  aliondoka  uwanjani  akichechemea   mchezo  ukiwa  bado dakika  20  kumalizika  lakini  kocha  Roberto Martinez  alipuuzia wasi  wasi huo , akisema  hakuna  sababu  ya  kuwa  na  wasi  wasi kuhusu  hilo.

Mwandishi: Sekione  Kitojo / afpe

Mhariri: Mohammed Abdul Rahman