1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Ujerumani kukata tikiti ya kombe la dunia

11 Oktoba 2013

Timu ya taifa ya Ujerumani itajihakikishia nafasi ya kushiriki michuano ya Kombe la dunia mwakani nchini Brazil kwa ushindi dhidi ya timu ya taifa ya Ireland katika mechi inayofanyika leo (11.10.2013)mjini Cologne.

https://p.dw.com/p/19yKx
Teamfoto / Mannschaftsbild / Mannschaftsfoto Deutschland: Hinten v.l.: Torwart Manuel NEUER (Deutschland), Per MERTESACKER (Deutschland), Toni KROOS (Deutschland), Miroslav KLOSE (Deutschland), Julian DRAXLER (Deutschland), Sami KHEDIRA (Deutschland), Jerome BOATENG (Deutschland). Vorne; v.l.: Kapitaen / Spielfuehrer / Mannschaftskapitaen Philipp LAHM (Deutschland), Thomas MUELLER (Deutschland), Marcel SCHMELZER (Deutschland), Mesut OEZIL (Deutschland). Fussball: Fussball-Nationalmannschaft der Maenner / WM-Qualifikationsspiel Deutschland - Faeroeer Inseln, Torshavn, Faeroeer Inseln, 10.09.2013 Football / Soccer: Germany/German National Football vs. Team Faeroe Island Torshavn, Faroe Islands, September 10, 2013. F?ßr??er-Inseln/WM-Qualifikation 2014
Timu ya taifa ya UjerumaniPicha: picture alliance/augenklick/GES

Hata matokeo ya sare yataiwezesha timu hiyo kushiriki fainali hizo kwa kutegemea matokeo ya mechi nyengine kwenye kundi lao ambalo lina timu za Austria, Sweden, Kazakhstan, jamhuri ya Ireland, Ujerumani na visiwa vya Faroe.

Katika mkutano na waandishi wa habari kabla ya kufanyika kwa mchezo huo ,kocha wa timu ya Ujerumani, Joachim Löw, amethibitisha kwamba kikosi chake cha kwanza cha wachezaji 10 kiko imara isipokuwa mchezaji mmoja wa kiungo upande wa kushoto, Marco Reus, ambaye ni majeruhi pamoja na mchezaji mzoevu wa timu ya taifa, Lukas Podolski.

KAISERSLAUTERN, GERMANY - AUGUST 14: Head coach Joachim Loew of Germany gestures during the international friendly match between Germany and Paraguay at Fritz-Walter-Stadium on August 14, 2013 in Kaiserslautern, Germany. (Photo by Alex Grimm/Bongarts/Getty Images)
Kocha wa timu ya Ujerumani Joachim LoewPicha: Getty Images

Wakati huo huo mchezaji chipukizi wa Uingereza Daniel Sturridge atakuwamo katika kikosi cha "Simba watatu " usiku huu kupambana na Montenegro katika uwanja wa Wembley baada ya kukosa mchezo wa kwanza mwezi uliopita dhidi ya Moldova kutokana na maumivu.

Sturridge ataungana na Wayne Rooney katika ushambuliaji baada ya kukosekana nae katika mchezo uliopita dhidi ya Moldova kutokana na maumivu.