1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

TOKYO: Uchaguzi wa baraza kuu la bunge nchini Japan

29 Julai 2007
https://p.dw.com/p/CBe7

Wajapani leo wanapiga kura kuchagua baraza kuu la bunge.Uchunguzi wa maoni uliofanywa hivi karibuni umeashiria kuwa serikali ya Waziri Mkuu Shinzo Abe,itashindwa vibaya sana.Wadadisi wanasema,Abe huenda akashinikzwa na chama chake cha Liberal Demokratik ajiuzulu,pindi chama hicho kitapoteza wingi wa kudhibiti baraza hilo,licha ya kuwa na wingi katika baraza dogo bungeni.

Umashuhuri wa Abe umepunguwa kwa sababu ya kashfa mbali mbali,ikiwa ni pamoja na ile inayohusika na malipo ya pensheni ya uzeeni.