1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

TOKYO: Chama tawala Japan chapoteza wingi

29 Julai 2007
https://p.dw.com/p/CBdy

Vyombo vya habari nchini Japan vinaripoti kuwa Waziri Mkuu Shinzo Abe anatazamia kubakia mdarakani.Hiyo licha ya matokeo ya mwanzo ya uchaguzi wa Baraza Kuu la Bunge,uliofanywa hii leo kuonyesha kuwa chama chake cha LDP kimeshindwa vibaya.

Wagombea kura katika uchaguzi wa leo hii wamepigania nusu ya viti 242 katika Baraza Kuu la Bungeni.Serikali ya mseto itabakia madarakani hata ikipoteza wingi wake katika baraza hilo kwa sababu ina wingi katika Baraza Dogo Bungeni.

Abe,alieshika madaraka miezi kumi iliyopita amepoteza umaarufu wake kwa sababu ya kashfa mbali mbali serikalini,ikiwa ni pamoja na ile inayohusika na malipo ya pensheni ya uzeeni.