1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

The Hague. Kamanda ahukumiwa kwenda jela miaka 26.

4 Novemba 2006
https://p.dw.com/p/CCw6

Mahakama ya kuwahukumu wahalifu wa vita nchini Bosnia imemhukumu kamanda mmoja wa wakati wa vita Mserbia kwenda jela miaka 26.

Marko samardzija , mwenye umri wa miaka 70 alikutikana na hatia ya kuamuru mauaji ya Waisamu 144 wakati wa vita vya Bosnia mwaka 1992-95.

Mahakama hiyo pia imemhukumu Mserb mwingine, Nikola Kovacevic , kwenda jela miaka 12 kwa uhalifu wa kivita dhidi ya Waislamu na Wakroati katika jimbo la jirani la Sanski.