1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Tetemeko dogo la ardhi Uingereza

27 Februari 2008
https://p.dw.com/p/DDux

LONDON:

Tetemeko dogo la ardhi limetokea nchini Uingereza likiwa na nguvu ya 4.7 katika Kipimo cha Richter.Kwa hivi sasa hakuna ripoti za hasara iliyosababishwa lakini watu wengi katika mji mkuu London na kwengineko walishtushwa usingizini.

Kiini cha tetemeko hilo lilitokea muda mfupi baada ya usiku wa manane,kilikuwa kama kilomita 80 mashariki ya mji wa Sheffield kaskazini mwa Uingereza.